Huduma za Wateja Maalum

Huduma za Wateja Maalum cover image

Huduma zetu za Wateja Maalum zinawahudumia watu mashuhuri wa hadhi ya juu na wagonjwa binafsi wanaopatiwa huduma katika vyumba vya binafsi wakiwa na madaktari bingwa na wauguzi maalumu waliowekwa kwa ajili yao. Wagonjwa hupata huduma kwa haraka katika mashauriano, uchunguzi na matibabu. Pia wanaweza kupanga miadi ya haraka, upasuaji na vipimo, kufurahia muda mfupi wa kusubiri na kupewa njia za kuingia na kutoka binafsi.

 

Faida za ziada

  • Huduma za ubingwa wa hali ya juu na mashauriano ya kitaalamu mbalimbali
  • Upasuaji siku hiyo hiyo

  • Huduma za uchunguzi wa haraka (Maabara na X-ray, Ultrasound, CT scan na MRI)

  • Ushauri wa daktari ndani ya dakika 10 baada ya kuwasili

  • Huduma za duka la dawa saa 24

  • Huduma za gari la wagonjwa saa 24

  • Chumba cha mapumziko cha viongozi (Executive Lounge)

  • Uongozaji kuanzia lango la kuingilia

  • Vinywaji (Maji safi, Kahawa, Chai na Juisi)

  • Malazi nafuu kwa wagonjwa wa kimataifa

  • Muda mfupi wa kupata majibu (TAT)

  • Wi-Fi ya bure

 

                                                                                KLINIKI YA "EXECUTIVE"

                          execeeeee.png

 

Kliniki ya Executive ipo ghorofa ya kwanza katika jengo la awamu ya kwanza. Kliniki hii imeundwa kutoa huduma za afya za ubora wa hali ya juu kwa wageni na wateja wanaohitaji huduma za kitaalamu kwa wakati na kwa hadhi ya juu.

Kliniki hii iko chini ya uongozi wa Daktari Bingwa wa Dharura (EMD) na hufanya kazi siku zote za wiki, kuanzia saa 2:00 asubuhi hadi saa 10:00 jioni siku za kazi (Jumatatu–Ijumaa), na saa 2:00 asubuhi hadi saa 8:00 mchana siku za mwisho wa wiki (Jumamosi–Jumapili).

 

Madaktari, wauguzi na wataalamu wengine waliobobea, wenye mafunzo ya hali ya juu na uzoefu mkubwa, huhudumia mgonjwa mmoja kwa wakati mmoja, wakizingatia mahitaji binafsi ya kila mmoja.

Kliniki hii ina vifaa vya kisasa kabisa, mifumo ya kielektroniki ya kuhifadhi taarifa za afya na mazingira rafiki kwa wagonjwa pamoja na familia zao.

 

 Kliniki ina:

  • Vyumba viwili vya ushauri (Consultation)
  • Chumba cha utaratibu wa matibabu (Procedure Room)
  • Vyumba viwili vya kungojea
  • Chumba cha uangalizi (Observation Room)
  • Vyoo vilivyo safi na vya kisasa

Sehemu ya kungojea ina burudani na vinywaji baridi ili kuleta hali ya faraja na utulivu, huku ukiruhusiwa kuendelea na kazi zako au kusubiri kwa subira hatua inayofuata.

 

Huduma na Maelekezo Muhimu:

  1. Wagonjwa wanaohitaji upasuaji wa siku hiyo hiyo (Day Surgery)uchunguzi wa moyo (Cardiac Evaluation) au kulazwa, watasindikizwa na kuhudumiwa kulingana na mpangilio wa huduma wa vitengo husika.
  2. Wagonjwa watakao kuwa wakisubiri huduma nyingine watatakiwa kuketi kwenye chumba cha kungojea, ambako watapewa vinywaji na vitafunwa kulingana na chaguo na mapendekezo ya daktari.
  3. Wakati wa kusubiri, kila mgonjwa atapewa kipeperushi cha mwongozo wa huduma, kitakachompa maelezo ya njia ya huduma na matarajio yake.
  4. Kwa maswali, maoni au miadi, tafadhali piga simu 0734331099 au tuma barua pepe kupitia info@bmh.or.tz
  5. Kwa lengo la kuboresha huduma na kuendeleza ubora, wagonjwa wataombwa kujaza dodoso fupi la maoni ili kuelezea kiwango ambacho hospitali imekidhi matarajio yao. Maoni haya hutolewa kwa hiari na yanathaminiwa sana.

Tunawatakia uzoefu wa kipekee na uponaji wa haraka ukiwa katika Kliniki yetu ya Executive. Faragha yako, usalama na afya yako ni kipaumbele chetu. Tuna utaalamu, uzoefu na vifaa vya kisasa vinavyotuwezesha kukuhudumia wewe na familia yako kwa njia bora, ya kitaalamu na kwa kutumia sayansi ya kisasa.

Kwa miadi au maelezo zaidi, wasiliana nasi kupitia +255 (0) 735000002.

 

                                                                         KLINIKI YA "PRIVATE -FAST TRACK"

Kliniki ya Fast Track ipo ghorofa ya pili ya jengo la awamu ya kwanza. Kliniki hii imeundwa kutoa huduma za afya kwa haraka, kwa uhakika na kwa ubora wa hali ya juu kwa wateja wanaoihudhuria.

Kliniki ipo chini ya uongozi wa Dkt. SAGUDA na Sr. NDOSI, na inafanya kazi siku zote za wiki kuanzia saa 2:00 asubuhi hadi saa 9:30 alasiri siku za kazi (Jumatatu hadi Ijumaa), na kuanzia saa 2:00 asubuhi hadi saa 8:00 mchana siku za mwisho wa wiki (Jumamosi na Jumapili).

Madaktari, wauguzi na wataalamu wengine waliobobea na wenye uzoefu mkubwa watakuwa wanahudumia mgonjwa mmoja kwa wakati mmoja wakizingatia mahitaji binafsi ya kila mmoja.

Kliniki imewekwa vifaa vya kisasa, mfumo wa kielektroniki wa kurekodi taarifa za wagonjwa, na imeundwa mahsusi kuunga mkono wagonjwa pamoja na familia zao. Kliniki ina vyumba vinne vya ushauri (Consultation rooms), chumba kimoja cha uangalizi (Observation), sehemu ya mapumziko (Lounge), Maabara ya kuchukua sampuli (Phlebotomy), Duka la Dawa (Pharmacy) na chumba cha Ultrasound. Sehemu ya kungojea ina runinga kubwa inayotoa elimu ya afya kila siku kuhusu masuala mbalimbali.

Tumejizatiti kutoa huduma salama zaidi, bora zaidi na yenye kuridhisha kwa kiwango cha juu, huku tukihakikisha unapata nafuu kwa haraka.

Taarifa Muhimu:

  1. Wagonjwa wanaohitaji upasuaji wa siku hiyo hiyo (Day Surgery), vipimo vya moyo (Cardiac Evaluation) au kulazwa, watasindikizwa na kuhudumiwa kulingana na mpangilio wa huduma wa vitengo husika.
  2. Wagonjwa walioko kwenye foleni watashauriwa wakae kwenye sehemu ya kungojea wakisubiri huduma inayofuata.
  3. Wagonjwa wote watapewa vipeperushi vyenye mwongozo wa huduma na maelezo ya nini cha kutarajia.
  4. Kwa maswali, maoni au nafasi ya miadi, tafadhali piga simu 0734331099 au tutumie barua pepe kupitia info@bmh.or.tz
  5. Kwa lengo la kuboresha huduma zetu na kuhakikisha ubora unaendelea kuimarika, wagonjwa wataombwa kujaza dodoso fupi kutoa maoni yao kuhusu huduma waliyopewa. Ushiriki ni wa hiari na unathaminiwa sana.

Tunawatakia uzoefu bora na uponaji wa haraka. Faragha yako, usalama na afya yako ni kipaumbele chetu. Tuna utaalamu na uzoefu unaohitajika kukupa wewe na familia yako huduma bora, ya kisasa na inayotegemea ushahidi wa kitaalamu na teknolojia ya kisasa kabisa.

Kwa miadi au maelezo zaidi, wasiliana nasi kupitia +255 (0) 735000002

 

          Mchoro wa Mtiririko wa Mgonjwa wa Huduma za 'Royal / Executive / Private-Fast Track'

                       Roya flow.png