USULUHISHI WA MIGOGORO
Tangu mwaka 1982 Baraza limekuwa likiratibu migogoro katika sekta ya ujenzi kwa njia ya usuluhishi. Baraza limeandaa orodha ya Wasuluhishi wa migogoro katika sekta ya ujenzi ambao husajiliwa na kutumiwa na wadau kwaajili ya usuluhishi wa migogoro inayojitokeza katika sekta. Aidha, utatuzi wa migogoro hufuata miongozo ya usuluhishi ambayo imechapishwa na Baraza.