Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wakala wa Majengo Tanzania (TBA)

WAUGUZI MBEYA RRH WAADHIMISHA SIKU YA WAUGUZI DUNIANI KWA MATEMBEZI NA MATENDO YA HURUMA

Imewekwa: 20 November, 2025
WAUGUZI MBEYA RRH WAADHIMISHA SIKU YA WAUGUZI DUNIANI KWA MATEMBEZI NA MATENDO YA HURUMA

Mbeya, Mei 12, 2025 — Katika kuadhimisha Siku ya Wauguzi Duniani, wauguzi kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya (Mbeya RRH) wamefanya matembezi maalum ya hamasa na kutoa huduma za huruma kwa jamii ikiwa ni sehemu ya shughuli zao za kijamii na kitabibu.

Maadhimisho hayo yameanza kwa matembezi ya amani kutoka Kabwe stendi hadi hospitalini.

Baada ya matembezi, wauguzi walitembelea wagonjwa waliolazwa wodini na kutoa huduma za huruma ikiwa ni pamoja na kuwafariji, na kuchangia Damu.

Muunguzi Mfawidhi wa hospitali, Bi. Maridhia Mvungi, alisema kuwa maadhimisho hayo ni fursa muhimu ya kutambua mchango mkubwa wa wauguzi katika mfumo wa afya na kuwaenzi wale wanaotoa huduma kwa moyo wa kujitolea.

"Leo tunasherehekea kazi ya wauguzi ambao ni uti wa mgongo wa sekta ya afya