Wakala Wa Huduma Ya Ununuzi Serikalini

"Ununuzi Unaozingatia Thamani"

Sisi ni Nani

Wakala wa huduma ya Ununuzi Serikalini (GPSA) ulianzishwa kwa mujibu wa Sheria ya Wakala Na. 30 ya mwaka 1997, kama ilivyorekebishwa kwa Tangazo la Serikali Na.235 la tarehe 7 Desemba, 2007. Wakala ulizinduliwa rasmi tarehe 16, Juni 2008. Wakala una ofisi katika Mikoa yote 26 Tanzania Bara na uko chini ya Wizara ya Fedha.