Huduma za mikopo

SIDO hutoa mikopo kwa wajasiriamali wadogo na wakati (SMEs) kwa ajili ya  kukuza mitaji ya miradi mbalimbali ikiwemo uwekezaji kwa watu binafsi au vikundi  kwenye sekta za biashara, uzalishaji pamoja na uwekezaji kwenye miundombinu ya biashara, zana na vifaa vya uzalishaji.

1.  AINA YA MIFUKO NA UTOAJI WA MIKOPO:-

SIDO hutoa mikopo hadi  shilingi  milioni 5 kupitia  mfuko wa kuendeleza Wajasiriamali Wananchi (NEDF) na  hadi   Shilingi  milioni 6. 5 kupitia mfuko wa mzunguko wa mkoa (RRF).  Pia SIDO kwa kushirikiana na benki ya CRDB PLC na Benki ya AZANIA LTD hutoa mikopo kuanzia shilingi milioni 7 hadi milioni 50, kupitia mfuko wa dhamana kwa Wajasiriamali Wadogo na wa Kati (Credit Guarantee Scheme) na kuanzia shilingi milioni 8 hadi milioni 500, kupitia mfuko wa SANVN (Viwanda Scheme)

A.   Mikopo kupitia mfuko wa dhamana (CGS) hutolewa katika mikoa yote Tanzania Bara kupitia Benki ya CRDB PLC na SANVN           (Viwanda Scheme) hutolewa katika  mikoa yote Tanzania Bara kupitia Benki ya   AZANIA LTD.

      Kipindi cha marejesho ni kati ya miezi sita (6)  hadi miaka mitatu  kwa mfuko wa NEDF, RRF na CGS.  Kipindi cha marejesho           ni hadi miaka saba (7) kwa mfuko wa SANVIN.

B.   Riba ya mkopo kwa mfuko  wa  NEDF ni asilimia 9 kwa mwaka  kwa miradi ya uzalishaji na  asilimia 12 kwa mwaka kwa                miradi isiyo ya uzalishaji.

C.   Riba ya mkopo kwa mfuko wa RRF ni asilimia 22 kwa mwaka kwa miradi ya uzalishaji.

D.   Riba ya mkopo kwa mfuko wa Dhamana ni asilimia 9 kwa mwaka kwa miradi ya uchakataji wa mazao ya kilimo  (Agro-                Processing)

E.  Riba ya mkopo kwa mfuko wa SANVIN ni asilimia 13 kwa mwaka kwa miradi ya sekta ya uzalishaji.

 2.   VIWANGO VYA MIKOPO

AINA YA MKOPO

KIWANGO CHA CHINI (TSHS)

KIWANGO CHA JUU (TSHS)

SEKTA

NEDF

-

 

-

1,000,000(Vikundi)

 

5,000,000

Biashara, huduma  ,

nyinginezo

Uzalishaji

RRF

-

6,500,000

 Uzalishaji 

CGS

7,000,000

50,000,000

Uzalishaji wa mazao ya kilimo

SANVIN

8,000,000

500,000,000

Uzalishaji

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

3.  MASHARITI YA MIKOPO

Masharti ya mikopo hayatofautiani sana kati ya mfuko mmoja hadi mwingine.   Lengo ni  kumwezesha mjasiriamali kuweza kuwekeza na kumpatia mtaji wa kufanya biashara

Mikopo hutolewa kupitia ofisi za SIDO - Mkoa  na mwombaji lazima awe ametimiza masharti    yafuatayo;-

(a) Mwombaji lazima awe na umri usiopungua miaka 18 na awe raia wa Tanzania.

(b) Mradi unaoombewa mkopo  lazima  uwe unakubalika kisheria, umefanyiwa upembuzi yakinifu wa kifedha na unakubalika                kijamii.
(c) Mradi   lazima uwe umesajiliwa kisheria,  mmiliki ana hati ya usajili wa jina la biashara na /au leseni halali ya biashara.

(d) Eneo la mradi liwe la  kudumu na kutambulika  na mamlaka za ndani.

(f) Mwombaji awe anatambulika  kwa viongozi wa mtaa husika  na  viongozi hao waoneshe utayari wa  kuthibitisha makazi na           uwepo wake  kwenye biashara husika.
(g) Mwombaji lazima  awe na nia ya kulipa mkopo husika.
(h) Mwombaji lazima awe na Akaunti Benki   yenye  jina la biashara husika.

(i)  Kwa mkopo wa mtu binafsi, mwombaji  lazima  awe na wadhamini  pamoja na  dhamana ya mkopo

(j)  Kwa mikopo ya vikundi, waombaji lazima wawe tayari kuunda kikundi na kuweka akiba ya asilimia 20 ya thamani ya mkopo          kama dhamana ya mkopo husika. 

(k) Kwa mfuko wa dhamana, mwombaji lazima awe amewahi kukopa SIDO au kupata huduma nyingine kama vile  teknolojia, mafunzo , masoko, ushauri wa kibiashara na ufundi au kupata huduma kupitia Programu mbalimbali zilizotekelezwa na SIDO kama vile MUVI KONGANO, KAIZEN n.k

(l)  Kwa mfuko wa SANVIN waombaji wawe Wajasiriamali waliohudumiwa na SIDO

 

Kwa maelezo zaidi waweza  kuwasiliana nasi

kupitia  ofisi ya SIDO ya mkoa iliyokaribu nawe au

kupitia anwani yetu hapa chini

 

Matangazo
03 Dec, 2025
23 Nov, 2025
Feedbacks

Mrejesho, Malalamiko au Wazo