Kurugenzi hii inahusika na ujenzi wa nyumba mpya za Serikali kwa ajili ya watumishi wa umma, Ujenzi wa nyumba mpya kwa ajili ya viongozi wa Serikali, Ujenzi wa majengo ya ofisi kwa Wizara na Taasisi za Serikali, Utengenezaji wa samani kwa ajili ya nyumba za makazi na Ofisi za Serikali na Ukarabati wa nyumba za makazi na majengo ya Ofisi za Serikali. Kurugenzi hii inaongozwa na Mkurugenzi akisaidiwa na Mameneja wa Sehemu mbili ambazo ni Sehemu ya Ujenzi na Sehemu ya Karakana na Matengenezo.