Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wakala wa Majengo Tanzania (TBA)

Kurugenzi ya Usimamizi wa Miliki

Kurugenzi hii ina jukumu la usimamizi na uendelezaji wa Miliki yote ya Serikali. Miliki ya Serikali ni pamoja na viwanja/maeneo ya ardhi yaliyotengwa kwa matumizi ya Serikali, Majengo ya ofisi za Taasisi mbalimbali za Serikali, nyumba za viongozi Serikalini na nyumba za kuuza na kupangisha kwa Watumishi wa Umma na Wananchi kwa ujumla. Idara hii inasimamiwa na Mkurugenzi akisaidiwa na Mameneja wa Sehemu tatu ambazo ni Sehemu ya Usimamizi wa Miliki, Sehemu ya Uendelezaji Miliki na Sehemu ya Usimamizi wa nyumba za Umma.