Kurugenzi hii inahusika na kutoa huduma za Ushauri kuhusu ubunifu majengo, uhandisi, ukadiriaji majenzi na huduma za majengo. Kurugenzi hii inaongozwa na Mkurugenzi akisaidiwa na mameneja wa sehemu nne ambazo ni Sehemu ya Ubunifu Majengo, Sehemu ya Uhandisi, Sehemu ya Ukadiriaji Majenzi na Sehemu ya Huduma za Majengo.