SHULE YA SEKONDARI YA WASICHANA KIBAHA
SHULE YA SEKONDARI YA WASICHANA KIBAHA
Shule ya Wasichana Kibaha
Shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaha (Kibaha Girls Secondary School), ni shule ya umma na ipo chini ya Kurugenzi ya Huduma za Elimu, Shirika la Elimu Kibaha (KEC). Shule hii ilianzishwa kwa ajili ya wasichana na ilisajiliwa mwaka 2007 kwa namba S.3880.
Huduma zinazotolewa
Elimu ya sekondari inatolewa kuanzia kidato cha kwanza mpaka cha nne kwa mchepuo wa masomo ya Sanaa, Sayansi na Biashara.
Mafanikio:
- Shule imefanikiwa kuwaendeleza wanafunzi kitaaluma na wamefanikiwa kujiunga na kidato cha tano na vyuo mbalimbali nchini.
- Shule ilishiriki katika mashindano ya ‘Tax club quiz competition’ kwa mfano mwaka 2023 shule ilikuwa mshindi wa tatu kitaifa.
- Shule ilishiriki katika mashindano ya miradi “projects” za “young scientists Tanzania” kwa mfano mwaka 2022 iliibuka na kuwa mshindi wa kwanza kitaifa.
Kujiunga na shule
Wanafunzi wanaojiunga na Shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaha, wanachaguliwa na Serikali.